Your Basket

Checkout | Shopping Cart
siri ya mvuvi mahiri || GetValue

SIRI YA MVUVI MAHIRI

SIRI YA MVUVI MAHIRI


Kila mvuvi mahiri huwa anajiandaa kabla ya kwenda ziwani au baharini kupata Riziki yake. 


Wapo waendao wakiwa na nyavu, wengine baruti, na wengine wakiwa na ndoano.


Kila mmoja huchagua njia aliyoizoea kwa kuzingatia kwanza aina ya Samaki anaowahitaji.


Wapo samaki anaowashika kwa kuwabembeleza, na wengine kwa Lazima hata kama hawataki.


KWA UPANDE WAKO 

Wateja wako wapoje ? 


Ni njia gani unazopaswa kutumia ili uweze kuwapata kirahisi ?


Sasa, 

Ili uweze kujua njia sahihi za kutumia, huna budi kumjua kwanza unayetaka kumpata. 


Saikolojia ya zamani ilikuwa inawafundisha wafanya biashara kujua anavyowaza Mteja kabla ya kununua bidhaa au huduma. 


Ila Saikolojia ya kisasa inakuhitaji mfanya biashara kujua kinachomsukuma Mtu kufanya maamuzi na kisha kununua unachokiuza.


Nyavu moja haiwezi ikanasa samaki wa kila aina; kwa Sababu waliyoitengeneza walizingatia kwanza aina ya samaki wanaotakiwa kunaswa na nyavu husika.


Na wala Huwezi kumshika Nyangumi kwa ndoano ya kumshikia Sangara au Sato.


Hivyo, kama mfanyabiashara au Mjasiriamali :


1. Watambue vizuri Wateja wako unaowahitaji 


2. Andaa Njia kadhaa za kuwanasa.


3. Waweke Wateja wako katika Makundi kadhaa kwa kulinganisha na Njia husika ya kuwanasa.


4. Anza na kundi moja baada ya jingine kwa kupima ni njia ipi inayozaa Matunda zaidi.


5. Jipatie kitabu changu cha "Mbinu 16 za kuongeza Mauzo kwenye Biashara Yako"; kitakachokusaidia sana katika kuyafanikisha yote hayo kwa Undani na kwa Uzuri zaidi. 


6. Wasiliana nami kwa nambari 0764793105 WhatsApp ili uweze kujipatia kitabu chako kwa Urahisi zaidi. 


P.S: Utapata 'Mentorship&Consultation'  ya BURE kwa Wiki nzima, pamoja na kitabu kingine cha BURE - Endapo utaizingatia hatua ya (5) ndani ya Saa 24 Tu, Siku hii ya Leo.


Kwanini upitwe!!


Huna haja ya kuendelea kupoteza Muda wako. Chukua Simu Yako ya mkononi, na kuicheki nambari 0764793105 WhatsApp. 


By LACKSON TUNGARAZA 

@lacksontungaraza 



Ratings: (0) Leave a Comment

You must login to post your comment.

Post Posting...